Tuesday, July 3, 2007

MWENYE MACHO AUZA PICHA YA KWANZA

Hatimaye Mwenye Macho ameuza picha yake ya kwanza katika maisha yake ya upigaji picha kwenye jarida moja huko Ufaransa kupitia wakala wa picha aitwaye Cedric Galbe. Cedric Galbe ni mpiga wa Kifaransa ambaye ameanzisha tovuti iitwayo http://www.galbe.com/. Tovuti hii ni wakala wa wapiga picha toka Africa, Scandinavia, Mashariki ya Kati, na Marekani ya Kusini.

Picha aliyouza ni hiyo hapo juu ya mtaalamu wa hesabu aitwaye Ron. Ron alitoa mada kwenye mkutano wa TED uliofanyika Arusha mwezi uliopita. Mada yake ilikuwa inaonyesha ni kwa jinsi gani hesabu zinavyothibitisha kuwa maisha yalianzia Afrika. Kwa habari zake zaidi tembelea http://www.jikomboe.com/, Ndesanjo alimwandika vizuri zaidi. Mimi sikumwelewa sawasawa kwani mimi na hesabu hatukuwahi kuwa marafiki hata kidogo.

Mpaka wakati mwingine, naelekea benki mara moja kuona kama dola zangu zimeingia.

3 comments:

mwandani said...

babu kubwa. endeleza mapambano.

Anonymous said...

hongera sana Sankofa

Đồ gia dụng said...

Thank you for sharing, if you handle the problem of office chairs. Please see the information below


sửa khoá két văn phòng
sửa khoá tủ văn phòng

sửa chữa bàn ghế văn phòng tại hà nội
sửa chữa ghế văn phòng tại hà nội