Wednesday, June 6, 2007

AFRIKA I TAYARI KWA BIASHARA.

Jukwaani yupo Carol Pineau. Yeye ni mwandishi wa Habari na mtengeneza filamu. Huyu yeye ameshatengeneza filamu kwenye maeneo yenye vita, njaa na migogoro mingine inayohusu Afrika hadi pale alipoamua "kuzaliwa upya" yani kutafuta mada chanya kwa ajili ya filamu zake. Sasa amegundua kuwa Afrika ina habari zingine pia na si matatizo tu. Filamu yake ya "Africa Open for Business" imempatia heshima kubwa sana ulimwenguni kote.

Kwa maneno yake mwenye akizungumzia filamu yake hiyo anasema, "It shows enterpreneurs in the one place no one expected to find them, Africa". Kweli hii ni Africa the next chapter.

Tafadhali tembelea tovuti yake, www.africaopenforbusiness.com. Hapa anatuonyesha sehemu ya filamu yake mpya itakayoitwa "Africa Investment Horizon".

No comments: