Wednesday, June 6, 2007

JANE GODALL NA SOKWE WA GOMBE

Jane Godall anatoa mada sasa. Ametusalimia kwa lugha zote yaani Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa, n.k. Lakini kuna hii moja, si mara yangu ya kwanza kumsikia akiitumia, ndio hasa iliyowachota watu hapa mkutanoni. Amesalimia kwa lugha ya sokwe.

Anaongelea mambo mengi kwa kweli, unaweza ukayaona kwenye www.jikomboe.com

Kuna kitu kimoja Jane anauliza, " Ni kwa nini leo binadamu anafanya maamuzi kwa kuangalia tu ni kwa jinsi gani maamuzi hayo yatamuathiri aidha kesho au kesho kutwa wakati babu zetu walikuwa wakifanya maamuzi si kwa kujiangalia wao wenyewe bali vizazi vyao vya baadae.

Alipokuja nchini mwaka 1960 kuanza maisha yake Tanganyika, msitu wa Gombe ulikuwa umenona na kulikuwa na sokwe milioni moja na ushehe sasa iweje leo msitu unakwisha na sokwe wamebaki takribani 150,000 tu. Anatuasa wanaTED kuwa katika kufikiria kwetu kuhusu mustakabali wa Afrika na maendeleo ya kiteknolojia hatuna budi kupigia kelele uharibifu unaosababishwa kwa kisingizio cha maendeleo ya teknolojia.

Kabla ya kutoa mada yake nilikutana na Jane asubuhi wenye chai ya saa nne. Nikaongea nae mambo kadhaa na hatimae nikafanikiwa kupata nilichokua nahitaji. Kumbukumbu, ambayo toka jan nilikua naikimbiza. Asante Jane!

No comments: