Wednesday, June 6, 2007

NDESANJO NDANI YA NYUMBA

Ndesanjo amefika juzi usiku. Ile natoka tu kwenye chumba cha mkutano namkuta akisalimiana na watu. Jamaa ni mtu mmoja safi sana. Picha hii nilimpiga jana, muda mfupi kabla Bi. Kidude hajalichakaza jukwaa la TED. Jamaa anablogu sio mchezo. Anaipenda kazi yake. Sasa jana jioni tulipotoka kwenye mkutano ndio akaniongoza katika tohara hii ya kuwa na blogu na hatimaye "Mwenye Macho..." imezaliwa. Asante Ndesanjo, japo jana sikulala hadi saa tisa usiku.

UHURU!

No comments: