Tuesday, June 5, 2007

UTANDAWAZI SOO!


Mkutano wa TED unafurahisha sana, nakaa natafakari kuwa sisi Watanzania tunaupokeaje utandawazi.

Hawa jamaa wako kwenye mgahawa wa Internet hapa Ngurudoto, Arusha, wanawasiliana na ulimwengu wote. Yani wanaupasha habari ulimwengu juu ya kile kinachoendelea hapa sasa. Kuna huyo dada hapo kushoto, ni rafiki yangu anaitwa Jen Brea, yeye ni mpiga picha pia. Tulikutana mtandaoni halafu tumekutana kwa mara yay kwanza "live" hapa Arusha. Yeye ni Mmarekani lakini anakaa Beijing, China. Nafikiri anawaandikia rafiki zake huko. Mcheki kwenye www.jenbrea.net

Kuna huyo bwana mweusi hapo kulia, yeye anaitwa David McQueen. Ni mwingereza. Yeye ni mtaalamu wa kufundisha watu kuzungumza mbele ya hadhira. Kama una tatizo la kuikabili hadhira mtafute jamaa fasta kwenye www.milestoneunltd.com. Jamaa anasema ana uzoefu wa kufundisha kwa miaka 20 sasa. Nilimfuma anachat na mkewe, anamwambia "Arusha safi sana!"

Hao wachina watatu sina habari zao ila nao wako kwenye TED.
Utandawazi unakutanisha jamii zote hata ubishe vipi.

No comments: