Thursday, June 7, 2007

USALAMA WA RAIS KWANZA

Yule rais kipenzi cha Watanzania, namaanisha Kikwete, ambaye muda wote anatabasamu, yani hata kama anakuadhibu tabasamu haling'oki, atakuwa hapa Ngurudoto leo ili kuufunga mkutano wa TED.

Hajafika bado na akitia timu tu (akiwasili) fasta namrusha hapa kwenye blogu. Dah! Ukiwa rais safi sana, yani huguswi, na uwezekano wa wewe kudhuriwa ni mdogo sana. Lazima niwe rais siku moja. Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu jinsi jamaa wa usalama wa taifa walivyokuwa wanatukagua leo kabla ya kuingia kwenye ukumbi, mi mwenyewe nikakoma. Manaake inabidi uonyeshe kila ulichonacho kwa usalama wa rais. Nikaanza kuwaza, sasa hawa jamaa si wanaweza wakatuambia tuvue nguo kabisa.

Baadae.

No comments: