Hajafika bado na akitia timu tu (akiwasili) fasta namrusha hapa kwenye blogu. Dah! Ukiwa rais safi sana, yani huguswi, na uwezekano wa wewe kudhuriwa ni mdogo sana. Lazima niwe rais siku moja. Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu jinsi jamaa wa usalama wa taifa walivyokuwa wanatukagua leo kabla ya kuingia kwenye ukumbi, mi mwenyewe nikakoma. Manaake inabidi uonyeshe kila ulichonacho kwa usalama wa rais. Nikaanza kuwaza, sasa hawa jamaa si wanaweza wakatuambia tuvue nguo kabisa.
Baadae.
No comments:
Post a Comment