Monday, June 18, 2007

ATI HII NI HAKI?

Jana majira ya jioni nilitoka kidogo kwenda kupata bilauri ya mvinyo na rafiki yangu mmoja anaitwa Sarah, jina la pili sitakupati kwa sasa, yeye ni mwandishi wa habari toka shirika la habari la Reuters (Hebu cheki vizuri, nimepatia speling?). Sasa katika blablaa zetu akanipa moja kali.

Ilikuwa siku ya Alhamisi iliyopita, alisafiri na ndege ya Precision Air akitokea Kilimanjaro kuja Dar es Salaam kupitia Zanzibar. Sasa kwenye ndege akaona ile inflight magazine ya ndege hiyo. Sarah anapenda kutengeneza pesa kwa kazi yake ya uandishi, hivyo alipofika pale Mwalimu Nyerere Airport fasta akakimbilia kwenye ofisi za hawa jamaa. Kufika pale jamaa wa pale ofisini full kumchangamkia Sarah, mzungu tena! (ndio Sarah ni Mmarekani)

Basi Sarah akaomba kuonana au kuongea na afsa mhusika, jamaa fasta wakamuunganisha kwenye simu. Sarah alikuwa anataka kujua yeye kama muandishi anaweza kuchangia makala kwenye magazine ya Precision Air. Afsa mhusika akamjibu kuwa anakaribishwa kwa mikono miwili, tena wana uhaba mkubwa wa wachangiaji (yani waandishi)

Sarah kusikia vile tabasamu likamjaa usoni, wale jamaa pale ofisini wakadhani anawatabasamia wao nao wakatengeneza tabasamu, kumbe mwenzao anafurahia opportunity. Sarah akajua hapa atatengeneza pesa ya kununulia mvinyo Dar.

Basi Sarah akaenda mbele zaidi, akamuuliza Afsa mhusika, "Enhe, huwa mnalipa shilingi ngapi kwa makala?" Afsa mhusika fasta akampa, "Huwa tunalipa kwa kila neno unaloandika...". Rafiki yangu Sarah akaona kweli dunia imekuwa tambarare 'yani hata Tanzania wanalipa kama Reuters!' (cheki tena speling aisee). Sarah kikamtoka kicheko kwa nguvu, wale jamaa pale ofisini nao wakaachia kicheko cha nguvu, sijui Sarah ana kicheko cha kuambukiza maana jamaa walikuwa hata hawajui mwenzao anacheka nini.

Basi Sarah akampa Afsa mhusika, "I think we can do business". Afsa mhusika nayeye akampa, "Definetly". Sarah akauliza, "Kwa hiyo mnalipa shilingi ngapi kwa kila neno moja la makala?", Afsa mhusika akampa, "Six to Ten Shillings". Sarah akapigwa na butwa asijue la kufanya, basi taratibu akarudisha kisemeo kwenye simu na taratibu akaanza kuondoka bila kuaga.

Sasa jana wakati ananipa kisa hiki akaniambia aliondoka bila kuaga si kwa kupenda bali kichwani alikuwa anajaribu kupiga hesabu kuwa makala yenye maneno miasita ingemlipa pesa ngapi, jibu likaja elfu sita. By the time anapata jibu alishawapita wale jamaa pale ofisini hivyo hakuwaaga.

Sasa hiyo elfu sita ambayo angelipwa ingemtosha kununua glasi mbili tu za huo mvinyo aliokuwa anakunywa na magazine inatoka mara moja kila mwezi. Sarah akaishia kuniuliza, "Bob, ati hii ni haki?". Sikuwa na jibu, labda wasomaji wa blogu hii mumsaidie.

2 comments:

Anonymous said...

Umenimaliza mbavu leo.

Bob Sankofa said...

Serina hayo ndio maswala ya kuwa mwajiriwa Bongo. Kaa vyema nnayo madude kama haya kibao