Wednesday, June 6, 2007

ROKIA ANAKUJA KUGAWA DOZI NYINGINE!

Siku ya kwanza inaelekea ukingoni. Lakini jamaa wa TED hawatuachi hivihivi, wanamrudisha tena Rokia Traore kwenye jukwa. Aisee natamani Ray C na Lady JD wangekuwa hapa wabadilishane mawazo na mtu huyu.

Anakamata gitaa lake sasa, pembeni yake kuna dada mmoja anaonekana kama mwenyeji wa Ethiopia hivi, ni mrembo we acha tu. Napata wasiwasi kidogo, sasa mbona hakuna mpiga drums, kinanda na vingine kama hivyo? Ahh! Kuna jamaa mmoja atapiga kinubi, halafu kuna mwingine ameshikilia kora.

Hebu subiri kwanza, hawa jamaa wanafanya utani, Bendi watu wanne!? Hapana mimi nimeshazoea hapa kwetu bendi watu kuanzia kumi na tano na kuendelea. Sijui, ngoja tusikilize.

Ayayayayaya! Ebwana si mchezo, huyu Rokia anaweza kusimama mwenye jukwaani bila hata kinubi na watu watapiga makofi. Dada anaimba bwana wacha. Kuna huyu jamaa anayepiga kora hapa, anatabasamu mwanzo hadi mwisho. Watu wanapenda kazi zao bwana.

Napiga picha hapa lakini nimekaa kimtegomtego, yani Rokia akishuka tu jukwaani nnae, nitasmile kidogo halafu ntampa, “May I have a photo with you please?”. Nasikia kiingereza hajui sana kwa hiyo hakutakuwa na mabishano marefu. Anatumia zaidi lugha yake ya asili lakini yuko mbali sana kuliko sisi tunaolazimisha lugha za wenzetu.

Nilijaribu kumtafuta Bono ila sijui alipotelea wapi. Jamaa yuko bize sana.

Rokia anamaliza nyimbo zake tatu na watu wanashindwa kubaki vitini, wamesimama kwa dakika kama moja na nusu hivi. Wakati wanaendelea kushangaa na kushangilia mimi najivuta kwa Rokia tayari kupata picha ya ukumbusho. Kumbe je, ntaonyesha nini wajukuu zangu? Tukutane siku ya pili.

No comments: