Friday, June 8, 2007

LEO NI KAMA KRISMAS

Ni muda wa mapumziko baada ya JK kutimka, watu wanapata chai ya saa nne asubuhi. Katika muda huu pia napata nafasi ya kukutana na rafiki yangu, mwanablogu, mwanzilishi wa Global Vioces, Ethan Zuckerman. Niliongea na Ethan jana akaniambia ameipenda sana blogu yangu na angependa kuona blogu nyingi zaidi za Kiswahili zikiibuka na yuko tayari kuzipa support. Watanzania tuandike kwa Kiswahili jamani, internet imepungukiwa lugha hii.

Nilisahau kukwambia kwamba leo asubuhi sisi washiriki miamoja tuliodhaminiwa na TED kuhudhuria mkutano huu, wakiwemo Watanzania kadhaa, tumezawadiwa laptops kila mmoja. Eti jamaa wanatuambia tuchague kati ya Mac au PC. Kula leki TED.

Samahani, sikufanikiwa kuwapiga watu picha walipokuwa wanashangilia kwani na mimi nilikuwa nashangilia pia. Ilikuwa nderemo na vifijo sio mchezo.

Pia kuna mtoa mada mwingine anaitwa Noah Samara, yeye ni mzakiwa wa Sudan lakini anaishi Marekani hivi sasa, yeye ndiye mwanzilishi na mmiliki wa radio ya WorldSpace. Yeye pia ameahidi wahudhuriaji 100 wakiwemo, Watanzania kadhaa, kwamba atawapatia radio hizo amabazo hupokea mawimbi yake toka kwenye satelait. Yani nitaweza kupata habari toka sehemu yeyote duniani, moja kwa moja. Ndio, hata Iraq pia!

Tafadhali soma zaidi habari hizi kwa Ethan (www.ethanzuckerman.com) na Ndesanjo (www.jikomboe.com)

No comments: