Wednesday, June 6, 2007

MAPUMZIKO

Duh, sio mchezo Watanzania. Tunapumzika sasa wana TED. Wenye kupata chai wakapate chai, wenye kupata kahawa wakapate na wenye kwenda kujistiri wakajistiri.

Mimi nazungukazunguka kutengeneza mtandao. Kwani nini maana ya mikutano? Ukienda kwenye mkutano halafu usitengeneze rafiki hata mmoja ujue mkutano umekushinda. Nzungukazunguka na nnakutana na Salim Amin, huyu ni mtoto wa Moh'd Amini, yule mwanahabari na mtengeneza filamu aliyeweka ukweli wa baa la njaa kule Ethiopia mwaka 1985. Salim amenichekesha sana, ananiambia baba yake walifanya kazi pamoja na Rais wetu msataafu miaka ile na baba yake alikuwa akimpa Mkapa lifti kweye skuta kila asubuhi.

Pia napata picha ya kumbukumbu na rafiki yangu David McQueen. Mwingereza huyu. Jamaa kila saa anaongelea jinsi anayomiss mkewe. Kula leki walai!

Kupumzika hakuna maana ya kulala ewe mwafrika, tengeneza mtandao kwani utandawazi uko mlangoni mwako! Tukutane ukumbini kwa ungwe ya pili.

No comments: