Wednesday, June 6, 2007

MAKAMUZI YANAENDELEA

Tumerudi baada ya mapumziko mafupi. WanaTED bila kupoteza wakati tunampandisha jukwaani mtengeneza filamu wa Kinigeria, lakini anayefanyia kazi zake Ulaya. Huyu anaitwa Newton Aduaka. Alikuwa anakaa London kwanza halafu sasa anakaa Paris. Kama kawaida yangu lazima nitamkamata tu ili nitwange nae "fotografia".

Anasema filamu zake anazotengeneza ni taswira ya maisha yake. Anatuonyesha vipande vifupi vya kazi zake kama nne moja ikiwa ni ile filamu ya "Ezra". Hii ni filamu inayoonyesha jinsi vita ya wenyewe kwa wenyewe ilivyoathiri Waafrika wa pale Sierra Leon. Anatuambia sisi kama Waafrika kabla ya kusonga mbele ni lazima tugeuke nyuma kwanza ili tusijerudia makosa. Filamu hii ilishinda zawadi kubwa ya tamasha la FESPACO pamoja na United Nations Peace Promotion Prize.


Tembelea tovuti yake www.planusa.org

No comments: