Tuesday, June 5, 2007

MCHAKAMCHAKA UNAANZA

Usifanye mchezo aisee, jamaa wa stage design ni kiboko. Huu ukumbi ukiingia humu unasahau kabisa kwamba kuna shida duniani. Jamaa wako kamili kila kitu kuanzia lighting, sound na mazagazaga yote. Ila duh! nasikia jamaa wa TED wamewaleta kutoka Afrika ya kusini. Hivi kwani Rita Paulsen na Benchmark yake si huwa wanafanya hizi kazi, sasa alikuwa wapi hakuchangamkia tenda hii atutoe Watanzania kimasomaso.

Aisee binadamu ni watu wa ajabu sana, katika zoezi la kuingia humu ndani hata watu wazima kabisa wanagombea nafasi za mbele. Si unajua tena. Na mimi nikiwemo :-)
Aisee nyie, hebu ngojeni kwanza! Otea ni nani anayeuanzisha mchakamchaka huu wa TED, aisee siamini, yani kwa macho yangu, kwa maana nyingine "live" namwona Rokia Traore stejini. Kama hujawahi kumsikia Rokia basi hujapata sikiliza muziki wa Kiafrika Magharibi wewe.

LAZIMA NIPIGE NAE PICHA, ROKIA WEEEEE! Kamua mama.

No comments: