Friday, June 22, 2007

MUNGU HULALA AFRIKA


Jana baada ya kukaa kwenye tarakilishi kwa masaa yasiyopungua kumi nikaamua kwenda ufukweni kusafisha macho, kama kawaida huwa sitoki bila SONY DSC-P32 mfukoni. Ni kamera ndogo na huwa nikiitoa mbele za watu wananicheka.


Sasa jana kwenye kutembea kwangu pembezoni mwa ufukwe wa Msasani (karibu na Sleepway) nikauona mwale wa jua uliochagua mmoja ya mitumbwi iliyokuwa imetulia baharini. Sijui nilifikiri nini, ila niliamini kuwa mwale ule una mahusiano na Mungu na pengine ni Mungu amemchagua mvuvi mwenye kumiliki mtumbwi ule ili ajisitiri kwa usiku ule. Sounds Crazy unhhh?!


Mungu hulala Afrika na pote pengine. Tafadhali tembelea picha zangu zaidi katika http://www.flickr.com/ , kule utanipata kwa jina la “babukadja”. Picha hii kwa kule nimeiita “God Sleeps in Africa”

2 comments:

Anonymous said...

Bob, get in touch with Chris Kabwato. I don't have your email address. Urgent. Tx

Bob Sankofa said...

OK, Thanks