Friday, June 15, 2007

UHURU NA VIDEO MKUNJUO

Nimetembelea blogu inaitwa http://www.onlinejournalismblog.wordpress.com/ nikakutana na habari hii "THE VIDEO JOURNALIST NEXT PURCHASE", Nikaona si vibaya nikiitafsiri kwa ndugu zangu wote wanaopenda teknolojia digitali, kublogu, pamoja na kiswahili.

Jamaa wanajiita Pure Digital Technologies, wametengeneza kajikamera haka kakurekodia picha za video na kuzirusha kwenye blogu yako kwa urahisi wa kupindukia. Wameipa jina la Flip Video (Video Mkunjuo). Jamaa wanadai kuwa wanataka swala la kublogu kwa picha na video lisiwe jambo la kutisha kiasi kwamba ukate tamaa na kuwaachia kazi hiyo watu kama kaka Issa Michuzi, au rafiki zangu Mjengwa na Mroki au Mwenye Macho.

Jamaa wa Pure Digital Technologies wanasema ni jukumu lao kuhakikisha kuwa wanatengeneza chombo hiki ili upashanaji wa habari za kiraia kwa njia ya video uwe rahisi na wa haraka kabisa. Kwa mawazo yangu ukiwa na hii kitu utaweza kuwatoa umaarufu CNN, ITV, BBC, FOX TV na wengine kama hao. Yani unaanzisha TV yako, kwa mfano Mwenye Macho TV.

Kamera hii inalingana na simu yako ya mkononi na inakuwezesha kukamata matukio bila kusumbuliwa na 'dola' wakati mwingine. Kwa mfano unaweza kurekodi jinsi askari wa jiji la Dar es Salaam wanavyokamata vyakula vya kina mama ntilie na kuvila wao wenyewe badala ya kuvipeleka vinakohusika. Jamaa wanaiuza kwa dola za kimarekani $129.99(bei ya kimatangazo hii) kwa maana nyingine ni $130.
Inasemekana kuwa hii ni kamera ya kwanza inayomwezesha mpiga video kuipiga video, kuihariri na haitamaye kuirusha video kwenye blogu bila kupoteza muda mwingi kwenye tarakilishi yako.

Wito wangu kwa wanablogu wa Tanzania, wapendao kublogu kwa picha na video, ni kuwa yatubidi kufanya mpango wa kupata hii kitu na kuanza kupashana habari kwa Waswahili waliomo ndani na nje ya nchi.

No comments: