Tuesday, June 5, 2007

DUH!

Aisee ni noma, mkutano bado dakika kadhaa uanze, yule mwanablogu mtukutu, Ndesanjo Macha hajatia timu. Ndesanjooooo! unaua bendi babuu. Niliposoma blogu yake siku ya tarehe 2 Juni kwamba jamaa wamemletea maroroso uwanja wa ndege huko ughaibuni hadi kusababisha jamaa kuikosa ndege nikajua anatania, si unajua wabongo kwa kupigana fix sometimes.

Haina noma sana lakini kwani ametuhakikishia kuwa hata kama ni kuikosa TED basi itakuwa kwa siku hii ya kwanza tu.

Watu ni lukuki hapa. Na kila mtu anaongea lugha fulani ambayo kwa namna fulani inahusihwa na tarakilishi (kompyuta), usipime mjomba.

Ahh! Hata Jane Godoll yupo. Nataka sana nipige nae picha aisee ila kila nikijisogeza kuna mtu anamuwahi. Bibi maarufu sana huyu. Atatoa mada kesho kuhusu sokwe na nyumba yao inayotoweka (msitu)

No comments: