Wednesday, June 6, 2007

HAPA NI DOZI JUU YA DOZI

Rokia amemaliza kutukaribisha, ameimba kwa lugha moja wapo ya kule kwao Mali. Wengi hatujaelewa neno kwa neno kwa kile alichoimba lakini kwa uelewa wa jumla amtukaribisha Afrika.

Inapita kama dakika moja na nusu halafu kwenye jukwaa anakaribishwa mwongozaji wa sinema na mpiga picha wa siku nyingi, bwana Andrew Dosunmu, yeye anatoka Nigeria. Ameshaongoza filamu ya "Hot Irons" (1999), ameongoza pia mchezo wa luninga huko Afrika ya Kusini uitwao "Yizo-Yizo". Ila katika kazi zote za huyu jamaa iko moja amabyo imenimaliza kabisa, yeye ndiye aliyetengeneza video ya muziki wa "Birima" wa Yossou N'dour. N'dour naye ilikuwa awepo hapa leo lakini ana shughuli za kibinafsi.
Dosunmu anasema wapiga picha na watengeneza filamu wa kiafrika tunawajibika kuonyesha upande wa pili wa maisha ya mwafrika kwa mtazamo wetu wenyewe, CNN na BBC na FOX TV hawalazimiki kufanya hivyo kwani kwao habari mbaya kuhusu Afrika ndiyo inayouza. Duh! Jamaa anaongea ile pidgin ya Kinigeria, simpati kila neno.

Nashindwa kujizuia, namsaka Dosunmu na kupiga naye picha. Tafadhali tembelea tovuti yake ya www.andrewdosunmu.com ujionee kazi zake.

No comments: